WELL COME TO GOLD MEDIA GROUP

WELL COME TO GOLD MEDIA GROUP
FILM PRODUCTION

Translate / tafsiri

Monday, December 9, 2013

TANZANIA YAAZIMISHA MIAKA 52 YA UHURU

Leo tar, 9.12.2013  Raisi J.M.Kikwete amewaongoza maelfu ya Watanzania pamoja na Wageni mbali mbali kutoka nchi za nje katika kuadhimisha Miaka 52 ya Uhuru Tanzania. Maadhimisho hayo yamefanyikia katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salam

                                         MATUKIO KATIKA PICHA 
 Raisi wa Jamhuri ya muungano akiwa na  Amiri Jeshi Mkuu  wa Tanzania wakiwasalimia Watanzania mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Uhuru Dar es salam

  Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya Tanzania wakipokea salamu ya Raisi na kupigiwa Mizinga 21 kutoka kwa Gwaride la Vikosi vya Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania leo katika Uwanja wa Uhuru mara baada ya kuwasili.
 Raisi wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania  na Amiri Jeshi mkuu wakikagua Gwaride la Vikosi vya Majeshi ya  Ulinzi na Usalama leo katika uwanja wa Uhuru wakati wa Maadhimisho ya Miaka 52 ya Uhuru
 Sehemu ya Vikosi vya Ulinzi na Usalama wakiwa wamesmama kwa Ukakamavu

 Baadhi ya Maofisa wa Jeshi wakipiga Saluti wakati Wimbo wa Taifa ukiimbwa


 Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania . akizungumza jambo na mkuu wa majeshi


 Gwaride likipita Mbele ya Raisi na Amiri jeshi mkuu kwa mwendo wa haraka


 Mke wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mama Salma Kikwete akiwasili Jukwaa Kuu la Uwanja wa uhuru katika Maadhimisho ya Miaka 52 ya Uhuru Tanzania.
 Maelfu ya Watanzania na Wageni  Waliohudhuria maadhimisho hayo
 Vijana wakiwasilisha Ujumbe kupitia Sanamu ya Mnyama aina ya Samba


 Vijana wakionyesha Ukakamavu Mbele ya Halaiki ya Watanzania na Wageni waliohudhuria Maadhimisho

 Raisi wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein {kushoto} Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mh,Jakaya Mrisho Kikwete {katikati}na Mkuu wa Majeshi Generali Mwamunyange wakisoma jarida letu lililochapishwa na idara ya habari
 Mheshimiwa Mbowe  ni mmoja wa Watanzania waliohudhuria Maadhimisho hayo akisoma Jarida la nchi yetu 


No comments: